Je! Biblia inasema nini kuhusu kucheza ngoma? Je! Wakristo wanapaswa kudansi?

Swali Je! Biblia inasema nini kuhusu kucheza ngoma? Je! Wakristo wanapaswa kudansi? Jibu Biblia haitoi maagizo maalum juu ya kucheza ngoma. Inaweza kuwa na manufaa kuelezea baadhi ya mifano ya kucheza ngoma vizuri na mbaya, na kisha kutaja kanuni za Biblia za kujenga viwango vya kucheza ngoma. Kutoka 32:6, 19-25-hii ni sehemu ya kusikitisha ya…

Swali

Je! Biblia inasema nini kuhusu kucheza ngoma? Je! Wakristo wanapaswa kudansi?

Jibu

Biblia haitoi maagizo maalum juu ya kucheza ngoma. Inaweza kuwa na manufaa kuelezea baadhi ya mifano ya kucheza ngoma vizuri na mbaya, na kisha kutaja kanuni za Biblia za kujenga viwango vya kucheza ngoma. Kutoka 32:6, 19-25-hii ni sehemu ya kusikitisha ya historia ya Israeli. Wakati Musa alikuwa juu ya mlima akizungumza na Mungu, Waisraeli walijenga sanamu. Katika mchakato wa ibada ya sanamu, walianza kucheza. Hii ilimalizia katika “shamrashamra” (mstari wa 6) na kuwa “nje ya udhibiti” (v.25 inasema “uchi” katika tafsiri zingine). Katika kesi hii, kucheza kunasababisha shughuli nyingi za dhambi. Katika Kutoka 15:20 Miriamu alikuwa akicheza kusherehekea ushindi wa nguvu za Mungu alileta katika Bahari ya Shamu. Samweli wa pili 6:12-16-Daudi “alicheza mbele ya Bwana” kusherehekea sanduku la Agano kurejeshwa Yerusalemu.

Kila mfano wa kucheza ambao hauonekani kuwa dhambi ulifanyika kwa ibada au sifa kwa Mungu. Hapa kuna kanuni zaidi za kukumbuka katika kuzingatia kucheza ngoma: Mhubiri 3:4-Kuna muda unaofaa wa kucheza (na kwa maana ya muda usiofaa wa kucheza). Zaburi 149:3; 150:4-vifungu vyote vinasema kuwa tunaweza kumsifu au kumwabudu Mungu kupitia kucheza. 1 Wakorintho 6:19-20 -miili yetu ni ya Mungu, na ni hekalu ya Roho Mtakatifu. Kwa hivyo kila kitu tunachofanya lazima tumheshimu Yeye.

Kucheza ili kuleta mvuto kwako mwenyewe au mwili wako kwa hivyo itakuwa dhambi. Katika 1 Wakorintho 7:1-3, mwandishi anasema, “Ni vyema kwa mwanaume asimguse mwanamke.” Paulo alikuwa akikubali kuwa wanaume wana hisia kali ya ngono ambayo ni rahisi kuanza. Kwa sababu ya hii, mitindo mingi ya kucheza nje ya ndoa inaweza kuwa ya kujaribu sana, hasa kwa mwanaume. “Kimbia [kama vile “kukimbia kutoka”] tamaa mbaya za ujana” (2 Timotheo 2:22). Dansi yoyote ambayo huchochea tamaa za dhambi ndani yetu au kwa wengine ni dhambi. Mathayo 18:6-kufanya kitu ambacho kinaweza kusababisha mtu mwingine kuanguka katika dhambi sio ya kusameheka kabisa. Kucheza kwa njia ambayo inaweza kusababishia mtu mwingine tamaa inaweza kuwa chini ya mwongozo huu. 1 Wathesalonike 5:22 — hii ni kanuni muhimu ikiwa hatujui kama hali ya kucheza inakubalika: “Jitengeni na ubaya wa kila namna.” Ikiwa inaonekana kama inaweza kuwa ya dhambi, usifanye hivyo.

Mwishoni, kuna kucheza kwingi ambao haufai kwa waumini wanapaswa kutafuta kumtukuza Mungu na maisha yao na miili yao. Hata hivyo Biblia inakubali kwamba tunaweza cheza kwa njia ambayo haijaribu wengine, haitujaribu wenyewe, na huleta utukufu kwa Mungu.

[English]


[Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili]

Je! Biblia inasema nini kuhusu kucheza ngoma? Je! Wakristo wanapaswa kudansi?

Similar Posts

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.