Je! Unaweza kuwa mchanga kiasi gani na kumwomba Yesu kuwa Mwokozi wako?

Swali Je! Unaweza kuwa mchanga kiasi gani na kumwomba Yesu kuwa Mwokozi wako? Jibu Hakika hakuna umri unaoitajika kwa wokovu. Yesu mwenyewe alisema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao” (Mathayo 19:14). Mara tu watoto wanapokuwa na umri wa kutosha kuelewa kwamba wamefanya dhambi (Warumi 3:23),…

Swali

Je! Unaweza kuwa mchanga kiasi gani na kumwomba Yesu kuwa Mwokozi wako?

Jibu

Hakika hakuna umri unaoitajika kwa wokovu. Yesu mwenyewe alisema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao” (Mathayo 19:14). Mara tu watoto wanapokuwa na umri wa kutosha kuelewa kwamba wamefanya dhambi (Warumi 3:23), kwamba Yesu alikufa kulipa adhabu ya dhambi zao (Warumi 5: 8; 6:23), na kwamba lazima waweke imani yao katika Yesu kwa wokovu (Yohana 3:16), basi wao wako na umri wa kutosha kuokolewa.

Mtoto hana haja ya kuelewa masuala yote magumu ambayo ni sehemu ya mafundisho ya wokovu. Ni muhimu kwamba wazazi wawe na hakika kwamba watoto wao wanaelewa masuala ya kimsingi (kama ilivyoelezwa hapo juu), lakini ahadi ya Matendo 16:31 ni sawa na kweli juu ya mtu mzima au mtoto: “Amini katika Bwana Yesu, nawe utaokolewa.”

Watoto wadogo, wazaliwa wa waumini au wasioamini, wanaweza kuchaguliwa na Mungu, wakakombolewa na damu ya Kristo, na kuwa na kazi ya Roho Mtakatifu ndani ya mioyo yao, na hivyo kuingia mbinguni. Kwa kiwango gani katika maisha yao wanafikia kutambua mambo haya yanatofautiana kutoka mtoto hadi mtoto. Baadhi ya watoto wadogo wana mioyo nyepesi na, baada ya kusikia kwamba Yesu alikufa kwa ajili yao, mara moja wanajua asili ya dhambi zao na wanalazimika kujibu. Wengine wenye tabia za kutumaini pengine hawawezi kutambua ufahamu huu hadi watakapokuwa wakubwa. Bwana tu anajua mawazo ya mioyo yao, na tunamwamini “kutafuta na kuokoa kile kilichopotea” (Luka 19:10) kulingana na mapenzi yake kamili na wakati.

[English]



[Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili]

Je! Unaweza kuwa mchanga kiasi gani na kumwomba Yesu kuwa Mwokozi wako?

Similar Posts

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.